YOUTUBE: TAKWIMU ZINAONESHA MUZIKI WA TANZANIA NDIO UNAOTAZAMWA ZAIDI NCHINI KENYA


Video za muziki wa Bongo Flava kutoka Tanzania ndizo zilizotazamwa zaidi na Wakenya katika mtandao wa YouTube, unaomilikiwa na Google, mwaka huu, takwimu zinaonyesha.
Video hizo zinatawala katika orodha ya video kumi zilizotazamwa zaidi, inayoongoza ikiwa video ya wimbo Salome, uliofanywa upya na Diamond Platnumz na Rayvanny.
Wimbo wa Work, wao Rihanna na Drake ni wa pili lakini kutoka hapo anaingia Diamond Platnumz na Harmonize wakiwa na wimbo wao Bado.
Video ya kwanza ya Wakenya kwenye orodha hiyo ni ya Sauti Sol kwa wimbo wao Unconditionally Bae, lakini bado kwenye wimbo huo walishirikiana na mwanamuziki Mtanzania, Alikiba
Hii ni hatua nzuri kwenye muziki wa bongo kwani inatoa matumaini na mwangaza kwamba ndio muziki  unaokubalika zaidi Afrika Mashariki.

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.