WAFAHAMU WAKWE NA KUKABILIANA NAO KATIKA KUONGOZA FAMILIA YAKO
Ni jambo jema kupatana na wakwe zako lakini ni vizuri kufahamu familia yako uendeshwa na wewe sio wakwe
KIKWAZO
“Mke wangu aliwaambia wazazi wake tulipokuwa tukikabili matatizo. Kisha baba yake akanipigia simu ili kunishauri jinsi ya kushughulikia hali hiyo. Sikufurahia jambo hilo!”— Joel machibya
“Mara nyingi mama mkwe husema, ‘Ninamkosa sana mwana wangu!’ Husema pia jinsi walivyokuwa karibu na mwana wake, jambo linalonifanya nihisi hatia kwamba nilifunga naye ndoa na kumletea mama yake maumivu ya moyo!”—Evelyn sankey
Je, inawezekana kuzuia hali ya kushughulika na wakwe isiwe tatizo katika ndoa?
UNACHOTAKIWA KUFAHAMU
Ndoa huanzisha familia mpya. Maandiko yanatuambia mwanamume anayefunga ndoa “atamwacha baba yake na mama yake naye atashikamana na mke wake.” Mke pia anafanya hivyo kuelekea wazazi wake na mume wake. Anapofunga ndoa, Pia maandiko yanatuambia kwamba wawili hao wanakuwa “mwili mmoja.” Wanaanzisha familia mpya.
Ndoa yako inachukua nafasi ya kwanza badala ya wazazi wako. Mshauri wa ndoa, John M. Gottman aliandika hivi: “Jukumu moja la msingi katika ndoa ni kwa mume na mke kuwa na umoja. Kuanzisha au kuchochea hisia hiyo ya kufanya mambo kwa umoja na mwenzi wako huenda kukatia ndani kutoshughulika sana na watu wa familia zenu.”
Huenda ikawa vigumu kwa baadhi ya wazazi kuzoea badiliko hilo. Mume mmoja kijana anasema hivi: “Mara nyingi mke wangu alitanguliza kutimiza mahitaji ya wazazi wake kabla ya ndoa yetu. Baada ya kufunga ndoa, mama yake aliona kwamba nafasi yake imechukuliwa. Haikuwa rahisi kwake kukubali hilo.”alizungumza bwana Rasuli mlekakule.
Huenda ikawa vigumu pia kwa baadhi ya wenzi wa ndoa wapya. Joel aliyenukuliwa mwanzoni anasema hivi: “Kuwa na wakwe si sawa na kuwa na marafiki unaochagua. Ni sawa na mtu fulani akuambie, ‘Umepata marafiki wawili wapya, iwe unapenda au la.’ Hata kama wanakuudhi bado ni sehemu ya familia yako!”
UNACHOWEZA KUFANYA
Ikiwa wewe na mwenzi wako hamwelewani inapohusu jinsi ya kushughulika na wakwe, jitahidini kurekebisha tatizo hilo kwa pamoja. Fuateni ushauri wa watu waliokuwepo kwenye ndoa mda mrefu na kuhusisha wazee maana katika jamii zetu tunaamini utu uzima ni dawa: ‘Tafuteni amani, na kuifuatia.
Ili kufanya hivyo, fikiria hali zifuatazo. Kila hali inaonyesha mtazamo wa mume au mke. Hata hivyo, wote wawili wanakabili changamoto zilezile na kanuni zitakazoonyeshwa zinaweza kuwasaidia kushughulika na wakwe.

Leave a Comment