KENYA: 30 NA ZAIDI WAFARIKI KWENYE MLIPUKO WA GARI AINA YA LORI
Idadi ya watu waliofariki katika ajali mbaya ya kuteketea kwa lori nchini Kenya, imepanda na kupata watu 30.
Kwa
mjibu wa naibu kamanda mkuu wa jimbo la Nakuru Isaaca Masinde, ajali
hiyo iliyotokea usiku wa kuamkia Jumapili katika eneo la Karai kwenye
barabara ya kutoka Nairobi kuelekea Naivasha.
Lori moja la kubeba
mafuta, lilianguka na kulipuka katika eneo la barabara hiyo yenye
shughuli nyingi nchini Kenya na kusababisha mauaji ya watu 30 papo
hapo.
Watu wengine zaidi wamefariki wakiwa kwenye matibabu mjini Naivasha.
Shirika
la msalaba mwekundu nchini humo, limesema lori hilo la mafuta,
lililokuwa njiani kuelekea nchi jirani la Uganda, lilipoteza usukani na
kisha kugonga magari kadhaa kwenye barabara kati ya Nairobi na Naivasha
yapata kimomita 100 kutoka mji mkuu Nairobi.
Leave a Comment