WAZUNGU WALIOMWEKA KWENYE JENEZA MTU MWEUSI WAFIKISHWA MAHAKAMANI AFRIKA KUSINI
Mtu mweusi nchini Afrika Kusini
ambaye alidaiwa kulazimishwa kuingia katika jeneza na wakulima wawili
weupe kwa kupita katika shamba lao amesema kuwa anahofia maisha yake.
Victor
Mlotshwa alikuwa akizungumza nje ya mahakama ya mji wa kaskazini
mashariki wa Middelburg ambapo waliotaka kumshambulia waliwasilishwa
katika mahakama.
watuhumiwa Theo Martins Jackson na Willem Oosthuizen
''Nilidhani wataniua'',alisema.
Kanda ya video ya dakika 20 iliorekodi kisa hicho imekuwa ikisambaa katika mitandao ya kijamii nchini Afrika Kusini.
Mwandishi
wa BBC Pumza Fihlani huko Middelburg anasema kuwa ndani ya mahakama
hiyo ,washtakiwa hao ,Theo Martins Kackson na Willem
Oosthuizen,walisimama wakiwa wameinamisha vichwa vyao chini huku
waandishi wa habari na raia wakichukua picha zao.
Victor Mlotshwa akisikiliza kesi yake dhidi ya wazungu hao mahakamani
Wameshtakiwa kwa kumteka nyara na kumshambulia kwa lengo kumjeruhi vibaya.Hawajakubali ama kukana mashtaka hayo.
Wawili
hao wanazuiliwa hadi tarehe 25 Januari huku waendesha mashtaka
wakisema kwamba walihitaji muda zaidi kuchunguza ,ikiwemo kuthibitisha
video hiyo
Mamake bw Mlotshwa alijawa na hasira na kushindwa kujizuia wakati wa
kusikizwa kwa kwesi hiyo.Nje ya mahakama kulikuwa na kelele za wafuasi
wa vyama vikuu nchini humo huku #RacismMustFall ikisambazwa katika
mitandao ya kijamii.
Mama mzazi wa Victor akilia kwa uchungu baada ya kushindwa kuvumilia kitendo alichofanyiwa mwanae
South Africa ni nchi yenye watu wengi weusi (asilimia themanini 80%) lakini uchumi mkubwa wa nchi unashikiliwa na wasauzi weupe ambao ni asilimia ishirini tu (20%).




Leave a Comment