MWONGOZO NA MATUKIO MBALI MBALI YA UCHAGUZI MAREKANI


Wamarekani wanapiga kura kuamua atakayekuwa rais wao wa 45. Hapa ni mambo muhimu ya kufuatilia wakati wa uchaguzi.
Majimbo yote 50 pamoja na Washington DC (eneo ambalo halijatambuliwa kama jimbo) watapiga kura katika nyakati sita tofauti za uchaguzi.
Tofauti hii inatokana na ukubwa wa taifa hilo, ambapo majimbo yaliyo mashariki yatatangulia kupiga kura na yale yaliyo magharibi yatakuwa ya mwisho.
Lakini kinyume na demokrasia nyingi, anayeshinda kura nyingi kitaifa si lazima awe ndiye atakayeibuka mshindi.
Marekani huwa na mfumo tofauti wa uchaguzi ambapo mshindi anahitajika kushinda kura 270 za wajumbe kati ya 538 zinazoshindaniwa.


Maeneo mengi Marekani yatasubiri vituo vifungwe- sana kati ya 19:00 EST (24:00 GMT) na 20:00 EST (01:00 GMT) - kuanza kupokea matokeo na makadirio ya matokeo katika majimbo mbalimbali.
Hata hivyo, kijiji kimoja kwa jina Dixville Notch katika jimbo la New Hampshire, kina desturi ya kupiga kura usiku wa manane. Kijiji hicho kitakuwa kimetangaza matokeo yake hata kabla ya upigaji kura kumalizika katika maeneo mengine. Hilo litakuwa mwendo wa saa 00:01 EST (05:01 GMT).
Hapa ni baadhi ya mambo ambayo huenda yakatokea, kwa kutegemea wakati ambao vituo vya kura vitafungwa. Hata hivyo, kuna uwezekano wa kuwepo tofauti kidogo katika wakati wa kufungwa kwa matokeo.
BBC itakuwa inategemea makadirio ya mshirika wake Marekani, ABC, kwa sababu inaweza ikachukua siku kadha kabla ya kura zote kuhesabiwa.
Na kuhusu matokeo kamili? Kaa chonjo na simu yako au uwe macho kwenye runinga mwendo wa saa 23:00 EST (04:00 GMT). Ukiona huenda ukapitwa kwa sababu ya usingizi, unaweza kuweka kengele ya saa ya kukuamsha. Huo ndio wakati upigaji kura utamalizika pwani ya Magharibi mwa Marekani. Historia inaonesha huo ndio wakati mshindi hutangazwa. Ilikuwa kabisa wakati huo ambapo mshindi alijulikana mwaka 2008, na dakika 15 baadaye mwaka 2012
Vituo vya kura Pwani ya Mashariki vyafungwa na kuhesabiwa kwa kura kuanza.
Macho ya wengi yatakuwa jimbo la kushindaniwa la Virginia (kura 13 za wajumbe), ambalo lilimpigia kura Barack Obama mwaka 2008 na 2012 lakini awali lilikuwa la Republican.
Donald Trump akishinda huko, au amkaribie sana Hillary Clinton, itakuwa ishara kwamba huenda ukawa usiku mrefu kwa wafuasi wa Democratic, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC Amerika Kaskazini Anthony Zurcher.
Jimbo la Georgia (16) pia ni muhimu. Jimbo hilo limeunga mkono chama cha Republican tangu 1996, lakini ubabe wa chama hicho umekuwa ukipungua miaka ya karibuni.
Pia, kunatarajiwa makadirio ya matokeo kutoka jimbo la Indiana (11), nyumbani kwa mgombea mwenza wa Trump Mike Pence, Kentucky (8), South Carolina (9) na Vermont (3)
akadirio ya matokeo Virginia Magharibi (5), jimbo ambalo limeunga mkono Republican tangu 2000.

CHANZO CHA HABARI : BBC Swahili

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.