MSOME HAPA CHIEF ISSA, MTANZANIA ANAYEMILIKI MGAHAWA SWEDEN
Chief Issa
Mgahawa mkubwa unaotoa huduma za
chakula cha Kitanzania unaomilikiwa na mpishi maarufu duniani, Issa
Kapande `Chef Issa', umefunguliwa nchini Sweden na kuvunja rekodi ya
dunia.
Mgahawa huo ulizinduliwa na balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mh. Dora Msechu.
Balozi
Msechu alimpongeza Issa Kapande na mkewe kwa kufanikisha kuwapo kwa
mgahawa huo ambao umeweka rekodi kuwa mgahawa mkubwa kuliko yote ya
Kiafrika katika nchi za Ulaya.
Katika mahojiano, Mpishi Mkuu Issa Kapande alisema mafanikio yake
yanatokana na juhudi kubwa na nia aliyoiweka katika kujifunza na
kufundisha wengine katika mitandao ya wapishi wakuu.
Alisema akiwa
amefanyakazi katika nchi 17 na tayari akiwa na vitega uchumi nchini
alianzia nia ya kuwekeza Sweden mwaka 2009 wakati alipohamia nchini humo
akitokea Uswisi. Alisema alianza kwa kuomba vibali, lakini mchakato
kamili ulianza mwaka 2013."Tulilazimika kufanya utafiti kidogo" alisema
na kuongeza kuwa katika utafiti huo walihoji watu 300 na kujua mwelekeo
hasa wa shughuli yao unastahili kuwaje.
Katika kazi yake ya upishi, amebahatika kuwapikia watu mashuhuri
duniani, baadhi wakiwa Andrew Young, Mchungaji Jesse Jackson, Robert
Mugabe (Rais wa Zimbabwe), Paul Kagame (Rais wa Rwanda), Benjamini Mkapa
(Rais mstaafu wa Tanzania), Raila Odinga (Waziri Mkuu wa zamani wa
Kenya), Daniel Arap Moi (Rais Mstaafu wa Kenya), Waziri wa Mambo ya Nje
wa Marekani Bi. Hillary Clinton na mumewe Bill Clinton, Mke wa Rais wa
zamani wa Marekani Laura Bush.
Wengine ni Rais wa Zanzibar Dk. Ali
Mohamed Shein, mwigizaji Chris Tucker, Rais wa zamani wa Afrika Kusini
hayati Mzee Nelson Mandela, Koffie Olomide, Youssour ndour, Arsene
Wenger (Kocha wa Arsenal ya England), Gianluca Vialli (nyota wa zamani
wa Italia aliyewahi kuichezea na kuinoa Chelsea ya England), Rais wa
Congo DRC, Joseph Kabila, Billy Gates na wengine wengi.


Leave a Comment