MPINZANI WA MUSEVENI NCHINI UGANDA KIZZA BESIGYE, AFANIKIWA KUONDOKA UGANDA


Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye ameandika kwenye mtandao wa twitter kuwa ameondoka nchini humo licha jitihada za serikali kumzuia.
Bwana Besigye aliliambia gazeti la Daily Monitor jana kuwa, alilazimika kufuta safari yake kwenda nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne kufuatia hatua ya polisi ya kuweka kizuizi nje ya nyumba yake.
Hata hivyo msemaji wa polisi alikanusha madai hayo.
Bwana Besigye anatarajiwa kuhutubia mkutano wa tume ya kimataifa ya mawakili mjini Johannesburg siku ya Alhamis.

PATA TAARIFA KWA WAKATI:
TEMBELEA PAGE ZETU ZA FACEBOOK, TWITTER NA INSTAGRAM ZINAZOPATIKANA KWA JINA LA "SIRI ZA JAMII" NA SUBSCRIBE KATIKA BLOG YETU KUPATA TAARIFA KWA WAKATI.

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.