MANCHESTER UNITED KUMWONGEZEA IBRAHIMOVIC MKATABA WA MWAKA MMOJA


Manchester United imesema kuwa itamuongezea mkataba wa mwaka mmoja mshambuliaji wake Zlatan Ibrahimovic kulingana na meneja Jose Mourinho.
Mchezaji huyo wa Sweden mwenye umri wa miaka 35 alihamia Old Trafford katika uhamisho wa bure katika msimu huu akiwa na uwezo wa kuongeza mkataba huo kwa msimu wa pili. Amefunga mabao 17 katika michuano yote msimu huu.
Mourinho alisema: Tutaanda mpango wa kuongeza mkataba wake kwa mwaka mwengine .Baadaye anaweza kufanya atakacho.
Ibrahimoviv alisema: Najihisi vyema, ikiwa nitaendelea itakuwa mwaka mwengine.
Ibrahimovic aliyefunga mabao 62 katika mechi 116 akiichezea Sweden kabla ya kustaafu katika soka ya kimataifa mnamo mwezi Juni ,alikihama klabu cha PSG mwishoni ma msimu uliopita

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.