HILARY CLINTON AELEZEA MACHUNGU ALIYONAYO BAADA YA KUSHINDWA URAIS KWENYE UCHAGUZI MKUU MAREKANI
Mgombea urais wa chama cha
Democratic Hillary Clinton ameelezea masikitiko yake alipojitokeza
hadharani mara ya kwanza tangu ashindwe kwenye uchaguzi wa rais nchini
Marekani na Donald Trump wa chama cha Republican.
Bi Clinton, akihutubia mjini Washington DC amesema alikuwa hataki kutoka nyumbani tena.
Ameliambia shirika la kuwasaidia watoto wasiojiweza kwamba uchaguzi huo umewafanya Wamarekani wengi kutafakari.
Bi Clinton aliongoza kwa wingi wa kura za kawaida lakini akashindwa
kinyang'anyiro cha urais kupitia kura za wajumbe, ambazo ndizo huamua
mshidni wa urais.
"Sasa, nitakiri kwamba kuja kwangu hapa halikuwa
jambo rahisi," alisema alipokuwa akitunukiwa heshima na wakfu wa
Children's Defense Fund.
"Kuna nyakati kadhaa wiki hiyo moja
iliyopita ambapo nilitaka kujikunyata tu nikiwa na kitabu kizuri na
nisiwahi kutoka nje ya nyumba tena."
Aliendelea: "Ninajua wengi wengu mmevunjwa moyo sana na matokeo ya uchaguzi. Hata mimi, pia, zaidi kushinda ninavyoweza kueleza.
"Ninajua
si jambo rahisi. Najua wiki moja iliyopita, watu wengi wamekuwa
wakijiuliza iwapo Marekani ni nchi ambayo tumekuwa tukiamini ndiyo.
Leave a Comment