DONALD TRUMP AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA KWENYE MGAHAWA MMOJA NCHINI MAREKANI NA KUSEMA MACHACHE
Rais mteule wa Marekani Donald Trump
aliwashangaza wateja, na wanahabari wanaofuatilia safari zake, baada ya
kujitokeza kwa kushtukiza katika mgahawa mmoja New York.
Wanahabari
waliopewa kazi ya kufuatilia safari zake walibaki kushangaa kwani
walikuwa wameelezwa kwamba angesalia nyumbani jioni hiyo.
Lakini
badala yake, aliandamana na kundi ndogo la maafisa hadi kwenye mgawaha
wa 21 Club katika mtaa wa Manhattan, moja ya migahawa anayoipenda sana.
Video zilizopigwa wakati wa kisa hicho Jumatano zinamuonyesha Bw Trump
akiwasalimia wateja na kuwaambia kwamba atapunguza kodi wanayolipa kwa
serikali.
Kwenye video, Bw Trump anaonekana akiwaambia wateja: "Tutapunguza kodi mnayolipa, msiwe na wasiwasi kuhusu hilo."
Kundi
la wanahabari waliopewa kazi ya kufuatilia safari za rais huyo mteule,
inadaiwa waliambiwa na msemaji wa Bw Trump, Hope Hicks, majira ya saa
18:45 kwamba alikuwa amekamilisha shughuli za siku na kwamba walikuwa
huru kwenda nyumbani.
Dakika 45 baadaye, msafara mkubwa wa magari
ulionekana ukiondoka kutoka ofisi kuu ya Bw Trump kwa sasa katika jumba
la Trump Tower. Msafara huo ulijumuisha magari zaidi ya kumi na gari la
kubeba wagonjwa.


Leave a Comment