BBC KUZINDUA IDHAA MPYA ITAKAYOTANGAZA KWA LUGHA 11


BBC World Service, kitengo cha shirika la BBC kinachohusika na utangazaji nje ya Uingereza, imetangaza kwamba itazindua idhaa 11 mpya katika upanuzi wake mkubwa zaidi kuwahi kufanyika tangu "miaka ya 1940".
Upanuzi huo unatokana na ongezeko la ufadhili lililotangazwa na serikali ya Uingereza mwaka jana.
Idhaa hizo mpya zitatangaza kwa lugha za Afaan Oromo, Amharic, Gujarati, Igbo, Korea, Marathi, Pidgin, Punjabi, Telugu, Tigrinya, na Yoruba.
Idhaa hizo mpya zinatarajiwa kuzinduliwa mwaka 2017.
"Hii ni siku ya kihistoria kwa BBC, tunatangaza upanuzi mkubwa kabisa wa World Service tangu miaka ya 1940," amesema mkurugenzi mkuu wa BBC Tony Hall.
"BBC World Service ni kito cha thamani kubwa - kwa BBC na kwa Uingereza.
"Tunapokaribia kuadhimisha karne moja tangu kuanzishwa, ruwaza yangu ni ya BBC yenye kujiamini na kufikia watu wengi zaidi, jambo ambalo litafikisha uanahabari wetu bora ulio huru, usioegemea upande wowote pamoja na burudani kwa watu nusu bilioni kote duniani.
"Leo ni hatua muhimu katika kutimiza lengo hilo."
"Lazima tuwafuate wasikilizaji na watazamaji wetu ambao siku hizi wanapata taarifa kwa njia mbalimbali, kwa kuongeza idadi ya watu wanaofuatilia taarifa za World Service kupitia TV, na huduma nyingi sasa ambazo zimeingia katika dijitali.
"Tutaweza kuharakisha mageuzi katika mfumo wa dijitali, hasa kuwalenga vijana na watoto, na tutaendelea kuwekeza katika taarifa zaidi za habari kwa njia ya video.
"Kile ambacho hakitabadilika ni kujitolea kwetu katika kuendelea uandishi wa habari huru na usioegemea uapnde wowote."
Upanuzi huu utahakikidha kwamba BBC World Service sasa inapatikana katika lugha 40, ikiwemo Kiingereza

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.