BBC KUZINDUA IDHAA MPYA ITAKAYOTANGAZA KWA LUGHA 11
BBC World Service, kitengo cha
shirika la BBC kinachohusika na utangazaji nje ya Uingereza, imetangaza
kwamba itazindua idhaa 11 mpya katika upanuzi wake mkubwa zaidi kuwahi
kufanyika tangu "miaka ya 1940".
Upanuzi huo unatokana na ongezeko la ufadhili lililotangazwa na serikali ya Uingereza mwaka jana.
Idhaa
hizo mpya zitatangaza kwa lugha za Afaan Oromo, Amharic, Gujarati,
Igbo, Korea, Marathi, Pidgin, Punjabi, Telugu, Tigrinya, na Yoruba.
Idhaa hizo mpya zinatarajiwa kuzinduliwa mwaka 2017.
"Hii
ni siku ya kihistoria kwa BBC, tunatangaza upanuzi mkubwa kabisa wa
World Service tangu miaka ya 1940," amesema mkurugenzi mkuu wa BBC Tony
Hall.
"BBC World Service ni kito cha thamani kubwa - kwa BBC na kwa Uingereza.
"Tunapokaribia kuadhimisha karne moja tangu kuanzishwa, ruwaza yangu ni
ya BBC yenye kujiamini na kufikia watu wengi zaidi, jambo ambalo
litafikisha uanahabari wetu bora ulio huru, usioegemea upande wowote
pamoja na burudani kwa watu nusu bilioni kote duniani.
"Leo ni hatua muhimu katika kutimiza lengo hilo."
"Lazima tuwafuate wasikilizaji na watazamaji wetu ambao siku hizi
wanapata taarifa kwa njia mbalimbali, kwa kuongeza idadi ya watu
wanaofuatilia taarifa za World Service kupitia TV, na huduma nyingi sasa
ambazo zimeingia katika dijitali.
"Tutaweza kuharakisha mageuzi
katika mfumo wa dijitali, hasa kuwalenga vijana na watoto, na
tutaendelea kuwekeza katika taarifa zaidi za habari kwa njia ya video.
"Kile ambacho hakitabadilika ni kujitolea kwetu katika kuendelea uandishi wa habari huru na usioegemea uapnde wowote."
Upanuzi huu utahakikidha kwamba BBC World Service sasa inapatikana katika lugha 40, ikiwemo Kiingereza


Leave a Comment