SCORPION MTOBOA MACHO AFUTIWA SHTAKA LILILOKUWA LIKIMKABILI
![[IMG]](https://www.jamiiforums.com/proxy.php?image=https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiIG31EqzoSThJRa1lLDk46MRn4HJgi3ep6p3MsjUfV-SPq1lcuXwajSpWm_OQIA-iLMi3c5BM8tT_6QyRFI-_dmf_We93Jyn533QLuE8FyC7KcVXDR20jnEgLw0D062efv8yqFDbqSv4ro/s400/NGE%25252BPICHA.jpg&hash=b25d9b675caed30a9303296c0076de1c)
Mahakama ya Wilaya ya Ilala, imemfutia shtaka linalomkabili mshtakiwa Salumu Njwete baada ya upande wa mashtaka kuomba shtaka hilo liondolewe mahakamani kwa sababu hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo.
Kutokana na maombi hayo, Hakimu Adelf Sachore amekubaliana na ombi hilo kwa kuzingatia kifungu namba 91 kifungu kidogo cha kwanza cha sheria ambacho kinampa Mamlaka Mkurugenzi Wa Mashtaka nchini (DPP) kuondoa shtaka mahakamani muda wowote ili mradi kama kesi hiyo haijatolewa hukumu.
Lakini kifungu hicho kinampa Mamlaka DPP kumshtaki mshtakiwa huyo endapo kama ana nia ya kuendesha shtaka hilo.
Njwete anakabiliwa na shtaka la unyang'anyi wa kutumia silaha na kumjeruhi Saidi Mrisho.
Lakini shtaka hili limefutwa hata hivyo anaweza kufunguliwa shtaka lingine.
Aidha, imeelezwa kuwa baada ya shtaka hilo kufutwa, upande wa mashtaka unatarajia kufungua shtaka jingine linalomkabili mtuhumiwa huyo.
Salum Njwete alifikishwa mahakani hapo akituhumiwa kumjeruhi Said Ally eneo la Buguruni kwa kutumia silaha ambapo inaelezwa kuwa alimuibia mali zake na kumtoboa macho yake.
Mtuhumiwa huyo bado anashikiliwa na Jeshi la Polisi.
Source :mwananchi.com
BLOG YA KIMATAIFA
ReplyDelete