RAIS MAGUFULI ATOA TAMKO KUHUSU MIKOPO YA WANAFUNZI VYUO VIKUU



Leo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa mabweni 20 ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 3,840 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Mwezi Juni mwaka huu wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa maktaba ya kisasa ya chuo hicho.

Wakati Rais Magufuli akiweka jiwe la msingi la mradi huo, tayari ujenzi umefikia asilimia 75 ambapo majengo 20 yaliyounganishwa kimuundo yamefikia ghorofa ya nne na ujenzi huo unaofanywa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 30 Desemba, 2016.

Rais Magufuli ameahidi kuwa, kwa kuwa majengo hayo yanauwezo wa kubeba ghorofa sita, Serikali itafanya utaratibu wa kutumia moja ya likizo za wanafunzi kuongeza ghorofa nyingine mbili ili kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kupata nafasi. Pia Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania alisema..
              "Vyuo vyote vya elimu ya juu viwe na tarehe moja ya kufungua, ukishafungua kwa haraharaka wakakaa pale kwa mwezi mmoja halafu unawaambia kufanya usajili lazima walipe wakati bodi haijatoa orodha ya majina ya vijana watakaokopeshwa, lazima kuwepo na mawasiliano kati ya bodi ya mikopo, TCU, wizara ya Elimu na wizara ya fedha"

        "lengo la serikali si kuleta usumbufu kwa wanafunzi, lakini ni ukweli pia haitatoa mkopo kwa wanafunzi wenye uwezo, mtoto wa Ndalichako naye apate mkopo?, mtoto wa katibu mkuu Kijazi naye apate mkopo? haiwezekani, mkopo huu umelenga kwa ajili ya kutoa watoto maskini lakini nasikia kule kuna upendeleo fulani katika kutoa mkopo sasa hili Waziri na bodi zinazohusike msimamie" John  Pombe Magufuli.

Raisi Magufuli akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa hostel ya wanafunzi katika chuo kikuu cha Dar es salaam
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania TBA Arch. Elius Mwakalinga akitoa ufafanuzi kwa Rais Magufuli kuhusu ujenzi wa Hosteli

1
Rais Magufuli akikata utepe kabla ya kuweka jiwe la msingi


5


Rais Magufuli na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandara

12

 ALICHOKIZUNGUMZA RAIS MAGUFULI KUHUSU MIKOPO YA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.