MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE: FAHAMU MAMBO 11 AMBAYO MWALIMU ALIYAPINGA NA KUKEMEA VIKALI
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere |
Alikuwa ni mototo wa chifu Burito Nyerere wa kabila dogo la wazanaki
Nyerere alifariki dunia kwa ugonjwa wa kansa ya damu, siku ya Alhamisi
Oktoba 14, 1999 saa 4:30 asubuhi [kwa saa za Afrika Mashariki], katika
hospitali ya Mtakatifu Thomas London, Uingereza akiwa amezungukwa na
timu ya madaktari bingwa.
Ndipo wananchi wote tulipigwa na butwaa kwa kumpoteza kiongozi mwenye msimamo thabiti na busara duniani.
Mwalimu bado ni taa inayong’aa gizani, umuhimu wake nazidi kuonekana kadiri miaka inavyokwenda licha ya kwamba amekwisha tuacha.
Wakati wa uhai wake Mwalimu Nyerere alichukia na kukemea vikali mambo
yasiyofaa kwa mustakabali wa maendeleo ya Tanzania , Afrika na Dunia kwa
ujumla. Baadhi ya mambo hayo ni:
1. UJINGA
Mwalimu
Nyerere alikuwa ni miongoni mwa wasomi wachache na ni mtanzania wa
kwanza kupata nafasi yamasomo ya juu katika Chuo Kikuu cha Edinburg ,
Uingereza na kuhitimu mwaka 1952 akiwa ni gwiji wa uchumi na historia.
Mwalimu
hakupenda ujinga na hivyo alipigana vita kali dhidi ya ujinga, na
alifanikiwa kwa nafasi yake kuwaondoa ujinga watanzania wengi, Ndiyo maana Rais Kikwete Februari
3, 2007 alisema “….sisi tuliwekezwa na ni lazima tuwekeze kwenu ili
miaka 30 ijayo Rais atoke miongoni mwenu….”
2. UBINAFSI NA UFISADI
Katika mambo aliyoyaamini sana na kuyapa mkazo wa aina yake, ni pamoja
na masuala ya haki na usawa. Mwalimu siku zote, alijenga imani katika
misngi ya utu, haki na usawa kwa kila raia wa dunia hii. Aidha Mwalimu
alipinga sana mianya ya unyonyaji aliyoiita ‘mirija’. Mwalimu alipinga
sera zozote zinazweza kuleta matabaka katika Taifa, iwe ni matabaka ya
kiuchumi kwa kuwa na kundi la walionacho na wasionacho.
Mwalimu hakuruhusu ubinafsi na ufisadi ambao ambao leo hii umekithiri miongoni mwa viongozi wengi hapa nchini.
Mwalimu aliwahi kusema “Hakuna mtu yeyote katika jamii atakayekuwa na
mahitaji yote muhimu wakati wengine katika jamii hiyohiyo hawana
chochote”.
Mwalimu alijikita katika siasa ya ‘ujamaa’ na kujitegemea na hatimaye
Azimio la Arusha mwaka 1967, ili kahakisha keki ya Taifa [National cake]
inakuwa na mgawanyo sawa kwa wote.
Mwaka 1978 nchi yetu ilikuwa katika wakati mgumu wa vita dhidi ya Nduli
Iddiamin Dada, lakini wabunge walihitaji nyongeza ya mishahara na
kupunguzwa posho ya waanafunzi wa elimu ya juu. Hali hii ilipelekea
wanafunzi wa enzi hiyo wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kugoma na kupinga
ubinafsi wa waung hao. Hapa tuliona msimamo, uzalendo na busara za
Mwalimu aliyetoa kauli kali ya kuamuru mishahara ya wabunge ipunguzwe na
posho za vijana zibaki kama awali.
3. UBEPARI
Mwalimu alikuwa ni nuru ing’aayo gizani, alipinga mfumo wa ubepari kwa
kuuita ‘mfumo wa ufukarishaji’. Hivyo aliimarisha misingi imara katika
itikadi yake ya ujamaa na kujitegemea, ikiwa ndiyo itikadi pekee yenye
misingi ya utu, haki na usawa.
Mwalimu alichukizwa sana na mfumo mpya wa kibepari uliozuka baada ya
yeye kung’atuka madarakani aliouita ‘ubepari wa pembezoni’ yaani ni
ubepari wa kishenzi unaotoa mianya kwa wachache kutumia mirija
kuwanyonya wanyonge.
Katika kitabu chake Ungozi wetu na hatima ya Tanzania ukurasa wa 28
Mwalimu alisema “Halimashauri kuu ya Taifa iliketi unguja, ikabadili
Azimio la Arusha bila kwanza kutafuta maoni ya wananchi, na walikuwa na
haki ya kufanya hivyo maana sera ni yao.Ubaya wao ni kwamba, jambo
lenyewe walilifanya kwa hila na janjajanja na mpaka sasa wanaendelea
kuwadanganya wananchi kwamba sera ya CCM ni ya ujamaa na Kujitegemea.”
4. UKABILA NA USEHEMU
Wakati Mwalimu Nyerere alipokuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam ,
alifanikiwa kuwaunganisha wanafunzi katika jumuiya moja iitwayo USARF
ikijumuisha wanafunzi kutoka nchi zote za Afrika. Aliona kuwa ni vema
kwani Afrrika ni moja. Leo hii wanafunzi wetu wanajitambulisha na
kujitanabaisha kwa makabila na sehemu watokazo.
USARF imekufa kabisa na imebezwa na vijikundi vya makabila yao .
5. UBINAFSISHAJI HOLELA WA MALI ZA UMMA
Wakati wa uhai wake Mwalimu alilaani vikali ubinafsishaji holela wa
masirika ya umma. Alwakataa Mabeberu waliojiita ‘wawekezaji’ walionuiya
kufirisi utajiri wa nchi yetu huku wakishibisha matumbo yao .
6. KUONGOZWA KWA RIMOTI NA NCHI MATAJIRI
Nakumbuka siku moja Mwalimu Nyerere akiwa katika viwanja vya mnazi mmoja
[Dar es salaam] aliwahi kusema “Tangu lini IMF ikawa International
Ministry of Finance?” [Wizara ya fedha ya kimataifa].
Leo hii viwanja hivyohivyo vinatumika kuusifu ubeberu wa IMF na
wawekezaji wake, huku tukiwekewa masharti magumu ya kuongoza nchi yetu
kwa maslahi ya mabeberu.
Mwalimu aliwaonya mataifa tajiri wasiingilie mambo yetu ya ndani, pale
walipoona maslahi yao hayazingatiwi, mara kwa mara walimuhoji Mwalimu
ambapo yeye aliwaamuru waondoke haraka na misaada yao yote.
Mwalimu hakupenda misaada ya kinafiki iliyolenga kuwaangamiza wananchi
wake, alipinga amri na maagizo ya taasisi za fedha kama Benki ya Dunia
[WB] na IMF [International Monetary Fund].Hivyo aliheshimu maamuzi yake
sahihi katika kulinda heshima ya nchi yetu na watu wake.
Kipindi chote cha uhai wake Mwalimu alisisitiza haja ya mataifa ya
Afrika kujitawala na kuwa huru katika kujiamulia mambo yake. “Inapotokea
taifa kuuza uhuru wake kwa ajili ya misaada ya kiuchumi au kukubali
kukaliwa na majeshi ya nje, taifa hilo linakuwa limepotea na litanyonywa
na watu wake watakuwa wanakandimizwa popote pale” alisema Mwalimu.
7. UBABE NA VITISHO KATIKA UONGOZI
Mwalimu aliamini kuwa kiongozi bora hapaswi kuwa na jazba na asiyetumia
ubabe wala vitisho katika maamuzi au katika kutatua tatizo ambalo jamii
inataka litatuliwe kwa maslahi na manufaa ya Taifa. Aliamini kuwa
kiongozi bora ni yule anayeruhusu mianya ya majadiliano baina yake na
wale anaowaongoza. Asiyetumia lugha chafu au kashfa na kejeli kwa watu
wake.
8. UMANGIMEZA NA UKIRITIMBA
Wakati wa uhai wake Mwalimu aliheshimu mipaka, taasisi za utawala na
mali za umma. Alichukia matumizi mabaya ya rasilimali za umma, pia
aliheshimu mawazo yake mwenyewe na ya wenzake.
Mwalimu aliamini kwamba, kiongozi asiyepeda ukiritimba na umangimeza ni
lazima awe mfuasi mzuri wa maadili anayoyasimamia, mwaminifu na
mwadilifu kwa manufaa ya Taifa lake. Mwalimu hakupenda kutetea uovu wa
viogozi eti kwa kutunza heshima zao au kulinda vyama vyao bila kujali
uhusiano wao wala majina yao . Hivyo katika serikali yake Mwalimu
hakuawa na ubia na mtu yeyote duniani.
9. USIRI WA MIKATABA NA MAKAMPUNI YA KIGENI
Mwalimu alisisitiza uwazi katika mikataba mbalimbali ambayo serikali iliingia na makampuni ya kigeni.
Katika kitabu chake cha Uhuru na Maendeleo Mwalimu anasema “Viongozi wa
kiserikali wana wajibu mkubwa wa kuwafahamisha wananchi nini serikali
inafanya na kwa sababu gain”
Tofauti kabisa hali ilivyo sasa, hali inayopelekea minung’uniko na
malumbano yanayo husisha hata ugawaji wa tenda za serikali. Labda
tuangalie mfano mmoja tu wa Mkataba wa Buzwagi ambao ulikuwa ni maarufu
kama ‘Mkataba wa Karamagi’ kati ya Waziri wa Nishati na Madini Nazir
Karamagi na Kampuni ya Barrik Gold Mine. Mkataba huu ulikuwa ni siri
kubwa baina ya Barrik na Waziri tu, hali iliyopelekea Mbunge Zitto Kabwe
kusimamishwa shughuli za bunge kwa miezi minne baada ya yeye kuhoji
uhalali na uharaka wa utiaji saini mkataba huo uliosainiwa hotelini
[Churchil Hotel] mjini London Uingereza.
10. RUSHWA
Katiba ya CCM katika ahadi yake ya nne [4] ina sema “rushwa ni adui wa
haki, sitatoa rushwa wala kupokea rushwa”. Jambo la rushwa pia Mzee wetu
mpendwa Mwl Nyerere alilikemea vikali enzi za uhai wake kwani alijua
wazi kuwa rushwa ni kikwazo cha maendeleo ya umma katika kila Taifa.
Nakumbuka Mh Kabuye [Mb-TLP] aliwahi kuwashutumu bungeni kuwa
anauhakika wabunge wote waliingia kwa rushwa, wabunge hao walioshutumiwa
walimtaka Kabuye afute kauli naye alisema “ kwa kulazimishwa nafuta
kauli”. Walimlazimisha lakini hoja yake ilibaki kuwa ni ya msingi.
11. UCHU WA MADARAKA
Mwl Nyerere ni miongoni mwa viongozi wachache sana duniani waliokosa
kuwa na uchu wa madaraka. Ni miaka 24 sasa tangu Mwl ang’atuke
madarakani kwa hiari yake akiwa kama rais wa awamu ya kwanza wa nchi
yetu na ni miaka 22 tangu aachie uongozi wa CCM kama Mwenyekiti wa
chama. Ndipo alipoamua kwa hiari yake kurejea Butihama na kuendeleza
kilimo.
Chanzo: Jambotz8
Leave a Comment