FAINALI ZA KLABU BINGWA ULAYA KUANZA KUCHEZWA NJE YA ULAYA

Michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya imekuwa ni kivutio kikubwa kwa mashabiki wengi wa soka ulimwenguni. Msimu huu pia umeanza na kasi kali kwa timu mbali mbali kupeana changamoto uwanjani na kuonesha uwezo wa kutunishiana misuli kwenye kabumbu.

 Bingwa Mtetezi wa michuano ya klabu bingwa ulaya Real Madrid, mapema Mei 2016
Katika kuboresha michuano hiyo, Rais wa Shirikisho la Soka barani ulaya (UEFA), Aleksander Ceferin raia wa Slovenia amesema bado analifuatilia shauri lake la kutaka fainali ya michuano hiyo kuchezwa nje ya Ulaya. Rais huyo amedai kwamba nchi mbali mbali zitatakiwa kutuma maombi ili kuwa wenyeji katika fainali hizo. Fainali zote 61 zilizochezwa kwa misimu yote zimechezwa ulaya, hivyo haoni shida ikiwa michuano hiyo ikachezwa kwenye miji mingine kama New York nchini Marekani au Beijing Nchini China.

 Rais wa Shirikisho la Soka Barani Ulaya (UEFA), Aleksander Ceferin
Aidha Rais huyo amelenga zaidi kukuza soko la mpira.  "Ukiangalia kifedha, hilo haliwezi kufaa. Lakini lazima tufikirie kuhusu masoko mengine pia. China inavutia kama soko, na Marekani pia. Soka inaanza kupata umaarufu huko pia," anasema rais huyo

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.