ARSENAL NA TOTTENHAM HOTSPURS WAINGIA KWENYE VITA KWA KUTUPA KARATA ZAO MPAKA MADRID

Arsenal na Tottenham Hotspur zapigana vikumbo kuipata saini ya Isco

Mahasimu wa London Arsenal na Tottenham Hotspur zimeripotiwa kupigana vikumbo kuiwaina saini ya Isco wa Real Madrid
Isco, 24, hana nafasi kwenye kikosi cha meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane na amecheza mara nne tu La Liga msimu huu, akiingia kutokea benchi dakika za mwisho kabisa.

Kwa mujibu wa chanzo cha Hispania Diario Madridista, mkataba wa Isco unafikia mwisho 2018 na Real Madrid wanashawishika kumuuza msimu ujao badala ya kumpa mkataba mpya.

Arsenal na Spurs ndizo klabu mbili anazoweza kujiunga nazo, kadhalika Manchester City ambayo pia imekuwa ikivutiwa naye kwa muda mrefu na kurejea Malaga unaweza kuwa moja ya karata anazoweza kuchagua.

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.