SERGE WAWA SASA YUKO FITI KUIKABILI RUVU SHOOTING

Serge Wawa akifuatilia kwa umakini mchezo wa Simba dhidi ya Azam


Azam FC itahitaji ushindi dhidi ya Ruvu Shooting katika mechi yao ya Jumamosi na kocha mpya Azam kwa mara ya kwanza atamtumia Serge Wawa
Kwa mara ya kwanza tangu kutua Azam kocha wa Azam FC Zeben Hernandez huenda Jumamosi hii akaanza kumtumia beki raia wa Ivory Coast Serge Wawa, ambaye amepona matatizo yake ya goti yaliyomweka nje tangu Aprili 2016 katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance ya Tunisia.
Daktari wa Azam FC, Mwanandi Mwankemwa amesema, kuwa Wawa ameanza mazoezi mepesi wiki mbili zilizopita na kwa sasa yupo fiti kwa ajili ya mikiki-mikiki ya ligi ya Vodacom Tanzania.
“Unajua tayari tumepoteza michezo miwili niwazi timu inaonekana kuwa na mapungufu hasa kwenye sehemu ya ulinzi sasa kupona kwa Wawa kunaweza kukawa msaada kwa kocha Hernandez ambaye kiukweli anaumiza kichwa kuona kikosi chake kinafanya vizuri,” amesema Mwankemwa.
Azam itapambana na Ruvu Shooting, kwenye uwanja wake wa nyumbani na itahitaji ushindi baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo dhidi ya Simba na Ndanda FC






s






No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.