PICHA :AJALI ILTOKEA KATIKATI YA MSAFARA WA MAKAMU WA RAISI MH SAMIA SULUHU AKIELEKEA MTWARA








Ni leo ijumaa ambapo Msafara wa makamu wa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh Samia Suluhu Hassani ambao ulikuwa unaelekea wilayani tandahimba ukitokea ikulu ndogo ya rais mtwara umepata ajali na kusababisha majeruhi ambao wamekimbizwa hospitali ya rufaa ligula.
Ajali imetokea mbele kidogo ya kijiji cha nanguruwe kilichopo halmashauri ya wilaya ya mtwara,majeruhi walioumia ni dereva pamoja na wasaidizi wanne wa makamu rais.
Gari hilo lililobeba wasaidizi wa rais kuacha njia na kupinduka, gari liliokuwa limebeba waandishi wa habari liliacha njia na nusura kupinduka.
Barabara ya kutoka mtwara kuelekea tandahimba si ya kiwango cha kuridhisha na kuruhusu magari kwenda mwendokasi hali iliyosababisha magari hayo kuacha njia na moja kupinduka kabisa na kusababisha majeruhi.


 .



 .




 .


.









No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.