NGASA AFUZU MAJARIBIO KUKIPIGA KWENYE CLUB YA OMAN

Baada ya kuachana na Free State Ngasa alitaka kurejea
Yanga lakini kocha Hans van der Pluijm, akamgomea na kuamua kutimkia
Oman ambapo amefanikiwa sasa
Ngassa aliyevunja mkataba wa kuitumikia Free State ya Afrika Kusini wiki tatu zilizopita ameiambia Goal, kwa njia ya mtandoa wa Fecebook, kwamba majaribio yake yalikwenda vizuri na amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo.
“Nashukuru majaribio yangu yalikwenda vizuri na kocha amekubali uwezo wangu na moja kwa moja amenipa mkataba wa miaka miwili hivyo kwasasa mimi ni mchezaji halali wa Fanja,”amesema Ngassa.
Baada ya kuachana na Free State Ngasa alitaka kurejea Yanga lakini kocha Hans van der Pluijm, akamgomea na kuamua kuitwa Oman kwa majaribio kwenye klabu ya Fanja na hatimaye amefanikiwa na sasa atajiunga na timu hiyo mara moja baada ya kukamilisha taratibu za kufanya kazi falme za kiarabu.

Leave a Comment