MKE WAKO ANAWAOMBA USHAURI WAZAZI KULIKO WEWE. NINI UFANYE? NIMEKUWEKEA HAPA NA MENGINE KUTOKA KWA MTAALAMU WA SAIKOLOJIA NA MAHUSIANO
Mke wako anasema kwamba angefurahi
ikiwa ungekuwa na uhusiano mzuri na mama yake. Lakini unaona ni vigumu
kushughulika na mama yake.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mke wako kuhusu tatizo hilo na uwe tayari
kufanya marekebisho. Jambo kuu si namna unavyohisi kuhusu mama-mkwe bali jinsi
unavyohisi kuhusu mwenzi wako uliyeapa kwamba utampenda. Wakati wa mazungumzo
mwambie njia moja au mbili hususa utakazotumia kuboresha uhusiano wako na mama
yake na ujitahidi kufanya hivyo. Kadiri anavyoona jitihada zako, mke wako
atakuheshimu zaidi.
MUME WAKO ANASEMA UNAWAANGAIKIA WAZAZI WAKO KULIKO YEYE.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mume wako kuhusu tatizo hilo ili kujua maoni
yake. Ni kweli kwamba mume wako hahitaji kuwa na hofu ya namna hiyo ikiwa
unawaheshimu wazazi wako. Hata hivyo,
unahitaji kumhakikishia kupitia maneno na matendo yako kwamba bado unamthamini
sana. Akiwa na uhakika huo, mume wako hatahisi kwamba anashindana na wazazi
wako ili tu umthamini
MKE WAKO ANAOMBA USHAURI KWA WAZAZI WAKE BADALA YA KUKUOMBA WEWE.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mke wako na mkubaliane kuhusu mambo
ambayo mnaweza kuomba ushauri wa wazazi. Jitahidi kuwa mwenye kukubali sababu.
Je, mara zote ni vibaya kuongea na mzazi kuhusu tatizo fulani? Ni wakati
gani unaofaa wa kuzungumza nao? Mkikubaliana kuweka mipaka yenye usawaziko,
hali hiyo haitakuwa tatizo.

Leave a Comment