MKE WAKO ANAWAOMBA USHAURI WAZAZI KULIKO WEWE. NINI UFANYE? NIMEKUWEKEA HAPA NA MENGINE KUTOKA KWA MTAALAMU WA SAIKOLOJIA NA MAHUSIANO




 Image result for husband and wife photos
Mke wako anasema kwamba angefurahi ikiwa ungekuwa na uhusiano mzuri na mama yake. Lakini unaona ni vigumu kushughulika na mama yake.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mke wako kuhusu tatizo hilo na uwe tayari kufanya marekebisho. Jambo kuu si namna unavyohisi kuhusu mama-mkwe bali jinsi unavyohisi kuhusu mwenzi wako uliyeapa kwamba utampenda. Wakati wa mazungumzo mwambie njia moja au mbili hususa utakazotumia kuboresha uhusiano wako na mama yake na ujitahidi kufanya hivyo. Kadiri anavyoona jitihada zako, mke wako atakuheshimu zaidi.
MUME WAKO ANASEMA UNAWAANGAIKIA WAZAZI WAKO KULIKO YEYE.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mume wako kuhusu tatizo hilo ili kujua maoni yake. Ni kweli kwamba mume wako hahitaji kuwa na hofu ya namna hiyo ikiwa unawaheshimu wazazi wako. Hata hivyo, unahitaji kumhakikishia kupitia maneno na matendo yako kwamba bado unamthamini sana. Akiwa na uhakika huo, mume wako hatahisi kwamba anashindana na wazazi wako ili tu umthamini
MKE WAKO ANAOMBA USHAURI KWA WAZAZI WAKE BADALA YA KUKUOMBA WEWE.
Jaribu kufanya hivi: Zungumza na mke wako na mkubaliane kuhusu mambo ambayo mnaweza kuomba ushauri wa wazazi. Jitahidi kuwa mwenye kukubali sababu. Je, mara zote ni vibaya kuongea na mzazi kuhusu tatizo fulani? Ni wakati gani unaofaa wa kuzungumza nao? Mkikubaliana kuweka mipaka yenye usawaziko, hali hiyo haitakuwa tatizo.

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.