MFUMO WA KUTUMIA KADI ZA KISASA NA SIO PESA MLANGONI KATIKA UWANJA WA TAIFA MKUU WAZINDULIWA

Baada ya kadi zilizotolewa za mwendo kasi hii ni hatua nyingine ya serikali katika kuongeza pato la nchi ambapo jumapili hii, waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye kwa niaba ya waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Majaliwa Kassim Majaliwa amezindua rasmi matumizi ya tiketi za kielektroniki katika uwanja mkuu wa taifa.
Mfumo huo
ni agizo la waziri Mh Kassim Majaliwa kuhusu udhibiti wa mapato kwenye
viingilio vya mlangoni ambapo ni mfumo utakaomtaka shabiki kuwa na kadi kama zile za benki ambapo atakuwa na uwezo wa kadi
yake aliyopewa kufanya manunuzi/malipo akiwa pia na uwezo kununua tiketi
za mechi atazopenda kupitia kadi hiyohiyo.
Miongoni mwa waliopewa kadi za kuingilia
uwanjani ni waziri Nape, Rais Magufuli na makamu wake mama Samia Suluhu
ikiwa ni uhamasishaji ambapo smartcard hiyo ya
kukuwezesha kuingia uwanjani itatolewa bure kwa shabiki na baada ya hapo
ataanza kuingia nayo uwanjani baada ya kuiwekea pesa.
Faida nyingine ya mfumo huo ni kuwa
hakutakuwa tena na utaratibu wa kugawanya mapato kwa njia ya mkono
kwenda katika taasisi husika ila ukikata tiketi asilimia za mgawanyo
zitakuwa zinafanywa kiteknolojia zaidi kwenda TFF, TRA, BMT katika kuliingizia taifa pato.

Leave a Comment