ZIDANE HATAJISIKIA VIZURI AKIYASIKIA HAYA KUTOKA KWA RONALDO


Ronaldo ameshindwa kuficha jibu lake kutokana na swali gumu aliloulizwa kwenye mkutano na waandishi wa habari baada ya kusign mkataba mpya na Nike. Kwenye moja ya maswali lilikuwa ni kocha yupo bora kwake kwa sasa hivi.
Jibu halikua gumu kutoka kwa Ronaldo,“Ni wazi kwamba makocha wangu wote wawili wamefanya kazi kubwa sana na timu zangu zote mbili Real Madrid na Portugal. Sasa kwa mawazo yangu ni ngumu sana kushinda ubingwa wa Ulaya na Portugal, ilikua ni mara yetu ya kwanza kwenye historia. “
Ronaldo aliendelea,“Zidane amefanya kazi nzuri sana lakini kwa sasa nampa favor Santos kama kocha bora. Hii haitokani kutokana na uhusiano wangu na hawa wawili. Wote nipo nao vizuri kabisa na wanafanya vitu vizuri kwangu. Lakini kwa sasa nampa Fernando Santos”

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.