MUNGU MWANAMKE WA INDIA APIGA WATU RISASI NA KUJERUHI HARUSINI

 Sadhvi Deva mwanamke anayejiita Mungu
Polisi nchini India wanamtafuta Sadhvi Deva Thakur, mwanamke aliye mafichoni baabda ya kufyatua risasi za kusherehekea kwenye harusi
Shaghaziye bwana harusi aliuawa huku watu wengine watatu wakijeruhiwa vibaya.
Kwenye video ya tukio hilo lililotokea siku ya Jumanne katia jimbo la Kaskazini la Haryana, Sadhvi Deva Thakur anaonekana akifyatua risasi akitumia bunduki aina ya revolver.
Mwanamke huyo alimuomba DJ kwenye harusi hiyo aupige wimbo anaoupenda huku akiendelea kufyatua risasi ndipo shangazi wa bwana harusi alianguka chini kwa kupigwa risasi na wengine watatu wamejeruhiwa vibaya.
Polisi wamewafungulia kesi ya mauaji na wanaendelea kuwatafuta wahusika saba wa tukio hilo.

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.