MAJARIBIO YA CHANJO YA UKIMWI KUFANYIKA AFRIKA KUSINI
Chanjo mpya dhidi ya virusi vinavyosababisha Ukimwi itaanza kufanyiwa majaribio nchini Afrika Kusini Jumatano wiki hii.
Wanasayansi wanasema huenda ikawezesha binadamu kukabiliana na virusi hivyo iwapo itafanikiwa, shirika la habari la AP linasema.
Wakati
wa majaribio hayo, ambayo yamepewa jina HVTN 702, wanasayansi
wanatarajiwa kuwatumia wanaume na wanawake 5,400 ambao wanashiriki ngono
kutoka maeneo 15 nchini Afrika Kusini.
Washiriki hao watakuwa wa umri wa kati ya miaka 18 na 35.
Majaribio
hayo yatakuwa makubwa zaidi na ya kina zaidi ya chanjo ya Ukimwi kuwahi
kufanyika nchini Afrika Kusini.
Leave a Comment