SHERIA YA HAKI MILIKI NA SHIRIKISHI NCHINI TANZANIA ITAMBUE HAPA


KATIKA mambo yanayowasumbua watu wengi duniani (Tanzania ikiwemo) ni suala la hakimiliki na hakishiriki kwa wasanii na wabunifu wa sanaa.Hapa nchini, baada ya sheria ya hakimiliki ya mwaka 1966 kuthibitika kwamba ina mapungufu mengi, ndipo mwaka 1999 Bunge la Jamhuri ya Muungano lilipotunga sheria mpya ya hakimiliki na hakishiriki, namba 7 ya mwaka 1999, yenye sura ya 218 ya sheria za Tanzania (kama zilivyorekebishwa mwaka 2002). 

Kwa mujibu wa utangulizi wa sheria hii, imeletwa kutengeneza na kutoa manufaa zaidi na ulinzi zaidi wa kazi za wasanii wa kazi zinazolindwa na haki miliki na hakishiriki na zingine zote zinazoendana na hizo.Chini ya kifungu cha 2(c) cha sheria hii, ambacho kimsingi kinazungumzia madhumuni ya kutungwa kwa sheria hii ya muhimu kwa maendeleo ya wasanii na watunzi na wabunifu wote katika nyanja za nyimbo, maigizo na tasnia nyingine zinazoendana na hizo.Sheria hii ina madhumuni ya kuinua kazi za fasihi na za kisanii pamoja na nyinginezo zinazofanana na hizo.

Kwa mujibu wa sheria hii, kuna makundi makubwa mawili ya haki za wasanii zinazolindwa na sheria hii, ambazo ni haki ya kiuchumi na haki za kitamaduni ambazo mtunzi wa kazi zinazolindwa na sheria hii ana haki nazo.

Haki hizi zina msingi katika mkataba wa kimataifa wa Benne wa mwaka 1883 ulioridhiwa na Tanzania Julai 25, 1994; na hivyo kwa mujibu wa kanuni za kisheria za kimataifa, Tanzania ina wajibu wa kutimiza yaliyomo katika mkataba huu iliyouridhia.Kwa mujibu wa sheria hii, chini ya kifungu cha 3(i) cha sheria hii, kazi zinazolindwa na sheria hii ni zile ambazo zimetengenezwa na mtunzi wa Kitanzania au zile ambazo mtunzi wake si Mtanzania lakini ana makazi yake ya kudumu hapa nchini au kazi hiyo iliyotengenezwa kwa mara ya kwanza hapa Tanzania, au kazi ambazo ni za kusikika na kuona (audio-visual) ambazo mtayarishaji wake ni Mtanzania au makao makuu yake yakutengeneza kazi hizo zipo nchini.

Na kwa mujibu wa kifungu cha 3(3) cha Sheria hii wasanii wanaomiliki kazi za kisanii na wana hakishiriki pia watapewa ulinzi na sheria hii.Katika kifungu cha 4, msanii ametafsiriwa kama mwigizaji, mwimbaji, mwanamuziki, mchezaji (dancer) au mtu anayeigiza, kuchonga au kufanya maonesho jukwaani.
Hata hivyo, sheria hii kama sheria nyingine nyingi za hakimiliki, imetoa sharti kwa kazi za kisanii kulindwa na sheria hii na kigezo hiki ni kwamba kazi hiyo iwe katika hali ya kushikika, na kwa maana nyingine ni kwamba wazo/mawazo hayatalindwa na sheria hii hata kidogo.

Kwa mfano, kama A na B walio katika sehemu tofauti lakini wana wazo linalofanana la kutengeneza wimbo unaohusu foleni za magari, na A akawa wa kwanza kuingiza wimbo huo katika hali ya kushikika (katika minajili hii akawa ameurekodi studio), basi B hawezi kuja kumshitaki A kwa kuiba wimbo wake kwani yeye alikuwa na wazo tu na wakati mwenzake aliliweka katika hali ya kushikika.

Hii ina maana kwamba, kazi ya kisanii haitalindwa na sheria hii kwa njia ya kusajili kazi hiyo, bali kwa njia ya kuiweka kazi yenyewe kuwekwa katika hali ya kushikika.
Kifungu cha 5 cha sheria hii kinaorodhesha baadhi ya kazi zinazolindwa ikiwa ni pamoja na kazi za sinema na michezo ya sinema, mihadhara, vitabu, majarida, kazi za muziki,upigaji wa picha za kawaida, ramani na picha za kuchonga na kadhalika. 

Kifungu hiki kinaendana na maamuzi ya Mahakama ya Uingereza katika shauri la University of London Press Ltd dhidi ya University Tutorial Press, (1916) 2 Ch.601 ambapo nayo ilitafsiri nini ni kazi ya kisanii kumaanisha yaliyomo katika kifungu cha 5 cha sheria ya hakimiliki na hakishiriki ya Tanzania.Kwa upande mwingine, sheria hii imetaja baadhi ya kazi ambazo haziwezi kulindwa na sheria hii ikiwa ni pamoja na habari zinazochapishwa/tangazwa katika vyombo vya habari, sheria na maamuzi ya vyombo vya kutoa maamuzi kama mahakama na mabaraza, na pia wazo la aina yeyote ambalo halijawekwa katika hali ya kushikika na kudumu, kama ambavyo wenzetu wa Uingereza walivyolipatia ufumbuzi katiak shauri la Springfield dhidi ya Temp, (1903) 19 TLR 650, ambapo mahakama iliamua kwamba wazo la aina yeyote haliko katika ulinzi wa sheria ya haki miliki wala hakishiriki.

Haki ya kiuchumi kama tulivyoona hapo awali, katika sheria ya Tanzania, inapatikana chini ya kifungu cha 9, na haki hii ni ile haki ambayo mtunzi wa kazi inayolindwa na sheria hii amepewa kuwa na haki zote juu ya kazi yake, katika masuala yote yanayohusiana na kutafsiri kazi yake, kuikodisha, kuionesha katika umma, kuionesha katika vyombo vya habari, kuisambaza, kuitumia hadharani na kadhalika. 

Haki hizi upatikana kwa kufata misingi ya sheria za nchi najua wewe anko wangu unaitaji kuwa msanii na kufanya kazi za sanaa na ndio maana anko wako nikaona nikusogezee kitu cha kuongeza ufahamu kama msanii na kukuza sanaa yako sio tu kwenye kipaji bali na kimaarifa pia.

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.