MUAMUZI MARTIN SAANYA KUAMUA MECHI YA SIMBA NA YANGA

Mwamuzi huyo ana beji ya FIFA na itakuwa mara yake ya
pili kuchezesha mechi kubwa ya Yanga dhidi ya Simba, mara ya kwanza
Yanga ilishinda mbili bila
Mwenyekiti wa Bodi ya ligi Boniface Wambura, amesema, wamemteua Saanya kuchezesha pambano hilo kwakua ana beji ya Shirikisho la soka duniani FIFA, na ana uzoefu mkubwa katika kuchezesha mechi kubwa kama hiyo.
“Tumemteua Saanya kwa sababu tunataka kumaliza utata mara nyingi timu hizi zimekuwa na malalamiko timu moja inapopoteza mchezo dhidi ya mwenzake na lawama kubwa hutupiwa mwamuzi sasa Saanya ana beji ya FIFA, tunaamini atachezesha vizuri na kila upande utaridhika,” amesema Wambura.
Hiyo itakuwa ni mara ya pili kwa Saanya kuchezesha mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga, mara ya kwanza alizichezesha timu hizo msimu wa 2013/14 na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
S
Leave a Comment