UMUHIMU WA KUANDIKA WOSIA

                            Posted by Erasto kachipa on tuesday, 30 August 2016
Pamekua na Migogoro mingi miongoni mwa wana jamii mpaka kufikia hatua ya kutoana maisha hasa baada ya mtegemezi kufariki dunia. Ndugu ugombania mali na ata watoto wa marehemu kudhuliwa na kukosa haki zao za msingi kama watoto wa marehemu na kutokujua nini cha kufanya baada ya mambo yote hayo kutokea. Na ndio maana Uncle wako leo nimeamua kukusogezea tiba ya tatizo kama ili kwa kukwambia njia pekee kwa mtu yoyote alie na familia moja ya jawabu sahihi ni kuandika wosia, japo vijana wa siku hizi wanalalamika kuwa wazee wao ni wakoloni kwamba kitendo cha kuandika wosia mzazi anaweza kuchukulia kama mtoto anamuombea dua mbaya lakini kwa dunia ya sasa watu inabidi waangalie  jamii ilipo kimaendeleo na kama kijana ni jukumu lako kutoa ushauri kwa mzazi au mlenzi kulinda mali zake zisipotee pindi anapokuwa ayupo kwa kuandika wosia.


    Najua wanajamii wenzangu mnachachu ya kufahamu nini maana ya wosia na jinsi gani ya kuandaa wosia basi ni muda pekee wa kukaa na mimi uncle wako na nitakuwekea kila kitu katika kilinge chetu cha siri za jamii

No comments

SIRI ZA JAMII. Powered by Blogger.